Wednesday, January 8, 2020

PREPARE THE WAY FOR THE LORD. PREPARE YOUR HEART FOR THE LORD.

Saturday, October 19, 2019

Swali: "Je, muumini anastahili kuwa na uwezo wa kuhisi Roho Mtakatifu?"



Jibu: 
Huku wakati wizara fulani za Roho Mtakatifu zinaweza kuhusisha hisia, kama vile hatia ya dhambi , faraja, na uwezeshaji, maandiko hayajatuamuru kuweka msingi wa uhusiano wetu na Roho Mtakatifu, jinsi gani au namna gani sisi tunahisi. Kila muumini aliyezaliwa mara ya pili amejazwa na Roho Mtakatifu. Yesu alituambia kwamba wakati Msaidizi atafika atakuwa nasi ndani yetu. "Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine ili akae nanyi hata milele ndiye Roho wa kweli, ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu” (Yohana 14:16-17). Kwa njia nyingine, Yesu anatuma mwingine moja kama yeye mwenyewe kuwa na sisi na kuwa ndani yetu.

Tunajua Roho Mtakatifu yu amoja nasi kwa sababu neno la Mungu linatuambia kwamba hivyo. Kila muumini aliyezaliwa mara ya pili amajazwa na Roho Mtakatifu, lakini si kila muumini anadhibitiwa na Roho Mtakatifu, na kuna tofauti maalumu. Wakati sisi tunachukua njia za kimwili wetu wa nje, sisi hatuko chini ya udhibiti wa Roho Mtakatifu ingawa sisi bado tumejazwa naye. Mtume Paulo atoa maoni juu ya ukweli huu, na yeye anatumia mfano ambao unatusaidia kuelewa. "Tena msilewe kwa mvinyio, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho"(Waefeso 5:18). Watu wengi husoma aya hii na kuitafsiri kuwa na maana ya kwamba mtume Paulo anazungumza juu ya mvinyo. Hata hivyo, mktadha wa kivungu hiki ni mwenendo na vita vya muumini aliyejazwa na Roho. Kwa hivyo, kuna kitu hapa zaidi ya onyo juu ya kunywa mvinyo sana.

Wakati watu wanalewa divai sana, wao huonyesha baadhi ya sifa fulani: wanakosa mawaziliano ya kimwili, hotuba yao ni ya ugugumizi, na hukumu yao ni uharibifu. Mtume Paulo anaweka ulinganisho hapa. Ni kama kuna baadhi ya tabia ambazo hutambua mtu ambaye anadhibitiwa na mvinyo, kuna pia tabia fulani kwamba hutambua mtu ambaye anadhibitiwa na Roho Mtakatifu. Tunasoma katika Wagalatia 5:22-24 kuhusu matunda ya Roho. Haya ni matunda ya Roho Mtakatifu, na ni ulioyanaonyeshwa na muumini ambaye amezaliwa mara ya pili ambaye ako chini ya utawala wake.

Kitenzi katika Waefeso 5:18 kinaonyesha mchakato endelevu wa " kujazwa " na Roho Mtakatifu. Tangu hili ni fundusho, kinachofuata ni kwamba kuna uwezekano pia wa kutojazwa au kudhibitiwa na Roho. Ufahamu mwingine wa Waefeso 5 unatupa sifa za muumini aioyoni mwenu; na kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo; hali mnanyenyekeana katika kicho cha Krist "(Waefeso 5:19-21).

Sisi hatuchajazwa na Roho kwa sababu tunahisi tumejazwa, lakini kwa sababu hii ni bahati na milki ya Kikristo. Kujazwa au kudhibitiwa na Roho ni matokeo ya kutembea katika utii kwa Bwana. Hii ni zawadi ya neema na si hisia. Hisia inaweza na hutudanganya, na tunaweza kufanya kazi wenyewe katika zile hisia mbaya ambazo zinatoka katika mwili na si za Roho Mtakatifu. "Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wal hamtazitimiza kamwe tama za mwili….Tukiishi kwa Roho na tuenende wka" ( Wagalatia 5:16, 25 ).

Baada ya kusema hayo, hatuwezi kukana kwamba kuna wakati tunaweza kuwa na kuzidiwa na uwepo na nguvu za Roho, na hii kwa mara nyingi huwa ni uzoefu wa hisia. hiyo inapotokea, ni furaha isiyo ya kifani. Mfalme Daudi "alicheza kwa nguvu zake zote" (2 Samweli 6:14) wakati wao walileta sanduku ya ahadi ya agano Yerusalemu. Kuhisi furaha na Roho ni kuelewa kwamba kama watoto wa Mungu sisi tumebarikiwa kwa neema yake. Hivyo, kabisa, huduma ya Roho Mtakatifu inaweza kuhusisha hisia zetu. Wakati huo huo, sisi hatustahili kuweka msingi wa uhakika wa milki yetu wa Roho Mtakatifu katika jinsi sisi tunavyouhisi.

Swali: "Je miujiza ya Roho Mtakatifu ipo kwa ajili ya siku hizi?"



Jibu: 
Kwanza, ni muimu kutambua kwamba hili si swali la ikiwa Mungu bado anafanya muijiza hii leo. Itakuwa ubumpavu, au swala lisilo la kibibilia kudai kwamba Mungu haponyi, haneni na watu, na hatendi miujiza na maajabu hii leo. Swali ni, ikiwa miujiza ya Roho Mtakatifu imeelezewa katika 1Wakorintho 12-14 kama bado haiko kazini katika kanisa hii leo. Pia hili si swali la kama Roho Mtakatifu anampa mtu miujiza ya Roho ya vipawa. Swali ni ikiwa Roho Mtakatifu bado anadhihirisha miujiza ya vipawa hii leo. Zaidi ya yote zote twatambua kwamba Roho Mtakatifu ako huru kudhihirisha vipawa kulingana na mapenzi yake (1Wakorintho 12:7-11).

Katika kitabu cha Matendo ya Mitume na Barua, wingi wa miujiza unafanywa na Wanafunzi na wendani wa karibu nao. Paulo anatoa sababu ni kwa nini: “Kweli ishara za mtume zilitendwa katikati yenu katika saburi yote, kwa ishara na maajabu na miujiza.” (2Wakorintho 12:12). Kama kila Mkristo katika Kristo alikua amejiami na uwezo wa kutenda ishara, maajabu na miujiza, kwa hivyo, ishara, maajabu na miujiza hivyo basi aingekuwa ishara ya mitume. Matendo ya Mitume 2:22 yatwambia kwamba Yesu “alisifiwa” kwa “miujiza, maajabu na ishara” vilevile, Mitume walitambulika kuwa watume wa kweli kutoka kwa Mungu kwa miujiza waliyoitenda. Matendo ya Mitume 14:3 yaeleza ujumbe wa injili “kuthibitishwa” na miujiza Paulo na Baranaba waliyoitenda.

Mlango wa 12-14 wa 1Wakorintho unashughulikia mada ya vipawa vya Roho Mtakatifu. Inaonekana kutoka kwa dondoo Wakristo wa “kawaida” wakati mwingine walipewa vipawa vya muijiza (12:8-10, 28-30). Hatwambiwie vile vilikuwa vya kila mara. Kutoka kwa kile tulicho kisoma kwamba mitume “walitambulika” kwa ishara na maajabu, inaweza onekana kuwa vipawa vya miujiza vilivyopewa Wakristo wa “kawaida” vilikuwa vya ihari si kwa mjibu wa sheria. Kando na Mitume na wale wendani wao wa karibu, Agano Jipya hakuna mahali kamili inamweleza mtu binafsi akitenda miujiza ya vipawa vya Roho.

Pia ni muimu kugundua kwamba kanisa la kwanza halikuwa na Bibilia iliyo kamilika, vile tuko nayo hii leo (2Timotheo 3:16-17). Kwa hivyo, vipawa vya unabii, maarifa, hekima na kadhalika vilikuwa vya muimu kwa sababu ya Wakristo wa kwanza wajue chenye Mungu anawahitaji wafanye. Kipawa cha unabii kiliwawezesha Wakristo kutangaza ukweli mpya na ufunuo kutoka kwa Mungu. Sasa kwa sababu ufunuo wa Mungu umekamilika katika Bibilia, ufunuo wa vipawa hauitajiki tena, kwa karibu lakini si kiwango sawa vile ilikuwa wakati wa Agano Jipya.

Kimuijiza Mungu huponya watu kila siku. Mungu bado hunena nasi hii leo, iwe ni kwa sauti inayosikika, kwa mawazo yetu au kupitia picha ya kimawazo au hisia. Mungu bado anatenda miujiza ya kushangaza, ishara na maajabu na wakati mwingine anatenda miujiza kupitia kwa Wakristo. Ingawa mambo haya si ya lazima, vipawa vya miujiza vya Roho. Lengo kuu la miujiza lilikuwa kuthibitisha kwamba injili ilikua ya kweli na mitume walikuwa watumwa wa kweli kutoka kwa Mungu. Bibilia haisemi wazi wazi kuwa vipawa vya miujiza vimetoweka, badala, yaweka mzingi, kwamba ni kwa nini havitaweza kutokea tena katika hali sawa na ile vilitokea wakati wa Agano Jipya.

Monday, September 23, 2019

YESU WA NAZARETI.

Kulingana na KAMUSI huru, ya WIKIPEDIA Yesu Kristo anajulikana kama ifuatavyo..

 inajulikana kama Yesu wa Nazareti na Yesu Kristo, alikuwa mhubiri wa Kiyahudi wa karne ya kwanza na kiongozi wa dini. Yeye ndiye mtu mkuu wa Ukristo. Wakristo wengi wanaamini yeye ni mwili wa Mungu Mwana na Masihi anayesubiriwa (Kristo) aliyetabiriwa katika Agano la Kale.  

Karibu wasomi wote wa kisasa wa zamani wanakubali kwamba Yesu alikuwepo kihistoria, [ingawa] kutaka kwa Yesu wa kihistoria kumetoa makubaliano madogo juu ya kuaminika kwa kihistoria kwa Injili na jinsi Yesu anavyoonyeshwa kwa karibu katika Bibilia huonyesha Yesu wa kihistoria.  Yesu alikuwa Myahudi wa Galilaya  ambaye alibatizwa na Yohana Mbatizaji na akaanza huduma yake mwenyewe. Alihubiri kwa mdomo  na mara nyingi alikuwa akiitwa "rabi". 

 Yesu alijadiliana na Wayahudi wenzake juu ya kufuata bora Mungu, kushiriki katika uponyaji, kufundishwa kwa mifano na kukusanya wafuasi. Alikamatwa na kushtakiwa na viongozi wa Kiyahudi,  akageuka kwenda kwa serikali ya Roma, na akasulubiwa kwa amri ya Pontius Pilato, mkuu wa Warumi.  Baada ya kifo chake, wafuasi wake waliamini kwamba amefufuka kutoka kwa wafu, na jamii ambayo waliunda baadaye ikawa Kanisa la kwanza.Mafundisho ya Kikristo ni pamoja na imani kwamba Yesu alichukuliwa na Roho Mtakatifu, alizaliwa na bikira anayeitwa Mariamu, alifanya miujiza, alianzisha Kanisa la Kikristo, alikufa kwa kusulubiwa kama dhabihu ya kufanikisha upatanisho kwa dhambi, akafufuka kutoka kwa wafu, na akapanda ndani Mbingu, kutoka atarudi.  Wakristo wengi wanaamini Yesu huwezesha watu kupatanishwa na Mungu. Imani ya Nicene inasisitiza kwamba Yesu atawahukumu walio hai na wafu ama kabla au baada ya ufufuko wao wa mwili, tukio lililofungwa kwa Kuja kwa Pili kwa Yesu katika eskatolojia ya Kikristo. 

 Idadi kubwa ya Wakristo humwabudu Yesu kama mwili wa Mungu Mwana, wa pili wa watu watatu wa Utatu. Wachache wa madhehebu ya Kikristo wanakataa Utatu, kabisa au kwa sehemu, kama isiyo ya maandiko. Kuzaliwa kwa Yesu kunadhimishwa kila mwaka mnamo Desemba 25 (au tarehe kadhaa mnamo Januari na makanisa kadhaa mashariki) kama Krismasi. Kusulubiwa kwake kunaheshimiwa Ijumaa Njema na ufufuko wake siku ya Pasaka. Enzi iliyotumiwa sana ya kalenda "AD", kutoka Kilatino anno Domini ("katika mwaka wa Bwana"), na mbadala sawa "CE", ni ya msingi wa siku ya kuzaliwa ya Yesu. 

Yesu pia anaheshimiwa katika dini ambazo sio za Kikristo. Katika Uislam, Yesu (kawaida hutafsiri kama Isa) anachukuliwa kuwa mmoja wa manabii muhimu wa Mungu na Masihi.  Waislamu wanaamini Yesu alikuwa mtoaji wa maandiko na alizaliwa na bikira, lakini hakuwa Mungu wala mwana wa Mungu. Korani inasema kwamba Yesu hakuwahi kudai uungu. Waislamu wengi hawaamini kuwa alisulubiwa, lakini kwamba aliinuliwa mbinguni na Mungu. Kinyume chake, Uyahudi unakataa imani kwamba Yesu ndiye Masihi anayesubiriwa, akisema kwamba hakutimiza unabii wa Masihi, na hakuwa mwungu wala hakufufuka.


NINI MAONI YAKO? Tuandikie hapa chini



Friday, August 30, 2019