Tuesday, August 20, 2019

ISRAELI NA ASEME SASA.

ZABURI 118 

1 Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele. 
2 Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.  
3 Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
  4 Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
  5 Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.  
6 Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?  
7 Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.  
8 Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu. 
 9 Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.

No comments:

Post a Comment